Read Msemakweli Sunday Christian Newspaper
|
Msemakweli
Sababu zinazofanya Wahindi, Waarabu wang’are
Na Mch. Nathaniel S. Kapela MORE..
Pamoja na Wapalestina kupinga ujenzi zaidi wa makazi ya Wayahudi katika eneo la Mashariki mwa Jiji la
Yerusalemu, Serikali ya Israeli imetangaza mpango mpya wa kujenga makazi 300 katika eneo hilo. Tangazo hilo
lililotolewa hivi karibuni, limekuja wakati ambao inahofiwa kuwa sio muafaka, kwa vile linaweza kuvuruga
mikakati ya amani kati ya Wayahudi na Wapalestina, inayotokana na mkutano wao uliofanyika wiki iliyopita
nchini Marekani.
Kwa mujibu wa Serikali ya Israeli makazi hayo mapya ya Wayahudi, yatajengwa katika eneo la Har Homa,
Mashariki mwa Jiji la Yerusalemu.
Eneo hilo licha ya kwamba ni miliki ya Serikali ya Israeli, linagombewa sana na Wapalestina kwa ajili ya kulifanya
makao Makuu ya taifa lao, wanaloamini kuwa siku moja litaundwa. Mara baada ya tangazo hilo la Israeli
kuchapishwa na kutangazwa katika Vyombo mbalimbali vya Habari, Maafisa wa Kipalestina walicharuka na
kuiomba Marekani kuzuia ujenzi wa makazi hayo. Nayo Israeli kupitia msemaji wa Serikali yake ilijibu kwamba
kamwe haitasitisha mpango wa ujenzi huo. “Ombi la kuzuia ujenzi huu, halina nafasi yoyote katika Jiji la
Yerusalemu”, Vyombo vya Habari vilimemnukuu mmoja wa wasemaji wa Serikali ya Israeli ambaye hakutajwa jina,
akisema. Hatima ya Jiji la Yerusalemu ambalo ni makao makuu ya taifa la Israeli, ni moja ya agenda ambazo
zinahofiwa kuvuruga mipango ya amani kati ya Wayahudi na Wapalestina, kutokana na kugombewa na pande hizo
mbili. Jiji hilo ni fahari na milki ya Israeli kwa sasa lakini Wapalestina wamekuwa wakilitaja kama sehemu ya milki
yao, na kwamba wanataka kulitwaa na kulifanya makao makuu ya taifa lao litakaloundwa baadaye. Israeli imekuwa
ikiyapuuza madai hayo ya wapalestina na kuyaelezea kuwa ni ndoto ya mchana ya mwendawazimu. Tofauti za
pande hizo mbili, zinazotia hofu juu ya hatma ya mazungumzo ya amani kati ya Wayahudi na Wapalestina. Katika
hatua nyingine, Televisheni ya Channel 2 nchini Marekani imeripoti kuwa Rais George Bush wa nchi hiyo,
anatarajia kufanya ziara nchini Israeli mwezi ujao. Ziara hiyo ni ya kwanza kwa Rais huyo tangu aingie madarakani.
Kwa mujibu wa Chombo hicho cha Habari, akiwa nchini humo, Rais Bush atazungumzia juu ya mchakato wa
amani kati ya Wayahudi na Wapalestina, sanjari na mradi wa nyuklia wa Iran.
Israel sasa kujenga makazi 300 Mashariki mwa Yerusalemu
Wapalestina wacharuka, wapinga vikali hatua hiyo
WAPO MISSION INTERNATIONAL
|